Monday 17 March 2014

Tusiruhusu ushoga nchini, hatari kwa taifa-Sheikh Muhenga



http://bloggerimports.files.wordpress.com/2008/12/img_2954-raisidd.jpg?w=640
Sheikh Mohammed Muhenga
SERIKALI imeombwa kufuata nyayo za serikali ya Uganda chini ya Rais Yoweri Museveni kwa kuktaa kuruhusu ushoga.
Serikali imeombwa kufuata nyayo za serikali ya Uganda chini ya Rais Yoweri Museveni kwa kukataa kuruhusu ushoga licha ya kuziudhi nchi za magharibi zinazokingia kifua vitendo hivyo.
Ombi hilo limetolewa na Imamu wa Msikiti wa Mwembechai, Sheikh Mohammed Muhenga, alipokuwa akiwahutubia waumini kabla ya swala ya Ijumaa iliyoswaliwa msikiti hapo, jijini Dar es Salaam.
Imamu Muhenga alisema kitendo cha Watanzania kunyamazia na kukumbatia matendo maovu yanayomchukiza Mungu vinaweza kuzua balaa kwa taifa.
"Tushirikiane kukemea maovu, tusinyamazie matendo yanayomchukiza Mungu kwani hakuna anayeweza kuhimili ghadhabu za Mungu akiamua kutuadhibu,"alisema .
Sheikh huyo alisema vitendo vya ulevi, biashara ya watu kujiuza, ujambazi na matendo mengine kwa kisingizio cha kukabiliana na hali ngumu ya maisha vinapaswa kuepukwa kwa nguvu zote.
"Huku ni sawa na kumbeep Mungu, je akiamua kutupigia tupo tayari kuhimili ghadhabu yake, tukemee maovu na kukemea kwani Mtume Muhammad (Sallallah Aley Wasalam) anasema miongoni mwa dalili 10 za kiama ni umma wake kugeuza pombe kuwa chai, watu kurejea enzi za Kaum Lut," alisema.
Sheikh alisema matendo vya ushoga na maovu mengine ni kuvuka mipaka kwa wanadamu ya uumbaji na humchukiza Mungu, hivyo ni wajibu wa kila mtu kukemea na kuyakataa matendo hayo.
Hivi karibuni Uganda ilipitisha sheria kali dhidi ya vitendo vya ushoga na kukera nchi ya Marekani na washirika kwake ambao wameruhusu vitendo hivyo katika nchi zao licha ya kwenda kinyume na mafundisho ya kidini.
Katika vitabu vya kuanzia Qur'an mpaka Biblia inasimulia kisa cha watu wa Nabii Lutu walivyotakabari na kuwaendea wanaume wenzao wakiwaacha wanawake na Mungu akawaadhibu adhabu inayoelezwa haijawahi kupewa wanadamu kama hiyo.

No comments:

Post a Comment