Monday 10 June 2013


SOMKI - FURSA YA UDHAMINI KWA AJILI YA WANAFUNZI WA KIKE WENYE VIPAJI LAKINI HAWAJIWEZI




Tunayo furaha kuwafahamisha kuwa kuna nafasi za udhamini kwa ajili ya wanafunzi wa kike wenye vipaji lakini wasiojiweza, chini ya Mradi wa Somesha Mtoto wa Kike (SOMKI). Mradi wa SOMKI unaleta utofauti katika maisha ya wanafunzi wa kike wa Tanzania wanaoishi katika mazingira magumu na wasiojiweza na ambao wameonyesha vipaji maalum au imeonekana kuwa na uwezo wa kufanya vizuri katika masomo yao na kufikia viwango vya juu au daraja la kwanza katika mitihani yao.

Udhamini huu ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba hawaathiriki na hali yao ya kimaisha ya sasa na kwamba wanaweza kupata fursa ya kubadilisha maisha na kuwa na maisha bora. Baada ya mchakato wa uhakiki na tathmini ya uhitaji itawapa walengwa fursa ya kupata elimu na kuwapunguzia mazingira magumu wanayoishi na kujisomea.

Tunaelewa kuwa katika shule yenu au utakuwa na taarifa kuwa kuna wanafunzi wanaostahili kupata nafasi hii. Kwa barua hii tunaomba uweze kusambaza taarifa hii na kuhamasisha wale wanaostahili kutuma maombi yao. Tafadhali nafasi hizi hutolewa mara moja tu kwa mwaka. Maombi haya yako wazi hadi kufikia tarehe 30 Desemba 2013, kwa ajili ya wanafunzi watakaodhaminiwa kitaaluma na Mradi wa SOMKI kwa mwaka 2014.

Maombi yatumwe kwenye anuani iliyopo hapo chini. Na kwa maelezo zaidi msisite kututafuta kwa anuani iliyopo hapo chini na namba ya simu.

Mlalakuwa,  Mikocheni,   Plot No: 36 B,   P.O. Box 71821, 
 Dar es Salaam, Tanzania 
Email: sophiamkana@yahoo.com Tel: +255-0656 647 280


Wenu mtiifu,

 Jane M


Mratibu wa Mradi 


No comments:

Post a Comment