Sunday 12 May 2013

Kongamano la Wanafunzi kufanyika Musoma



CONGAMANO
 
TAASISI ya kuhamasisha maendeleo na mawasiliano katika jamii yenye makao yake mjini Musoma mkoani Mara ya JAMII INFORMATION NETWORK inatarajia kufanya Kongamano kubwa litakalo wahusisha  Wanafunzi zaidi ya 200 kutoka Shule 10 za Sekondari za Manispaa ya Musoma Mwezi Agosti mwaka huu, ikiwa ni njia ya kuhamasisha Maendeleo na uimarishaji wa Mawasiliano ndani ya Jamii.
Katika Kongamano hilo mada mbalimbali zitatolewa na Wataalamu waliobobea katika Masuala ya uhamasishaji wa Vijana Kupambana dhidi ya Ukimwi,ujasiriamali,dhana ya kujiajiri,Changamoto katika Elimu kwa Vijana  pamoja na Ukatili wa Kijinsia ikiwa ni njia ya kujenga msingi bora wa makuzi kwa vijana wetu.
Mbali na hivyo vijana hao pia wataelezwa jinsi ya kuwa Wazalendo katika nchi yao,kupambana na rushwa,Umaskini lakini pia wakipata elimu sahihi ya faida za uwekezaji kwa Tanzania,Sababu za Mimba za Mapema kwa watoto wa kike na jinsi ya kujenga Mahusiano na Mawasiliano yaliyo sahihi.
Pamoja na Mtandao huu kuwa na nia njema katika kuwasaidia vijana lakini bado kumekuwepo na changamoto mbalimbali katika kufanikisha Kongamano hilo hasa katika Suala la kifedha,hivyo basi Taasisi ya JAMII INFORMATION NETWORK kwa nia njema inakuomba wewe Mtanzania,mpenda maendeleo,unaekaa ndani au nje ya nchi,Mashirika kusaidia taasisi hii katika kufanikisha kongamano hilo ili vijana wetu wakue katika makuzi mema na kujenga Tanzania ya kesho  iliyostaarabika.
Chanzo:Full Shangwe

No comments:

Post a Comment