Thursday 9 May 2013

Wajasiriamali wanawake kukutana Dar Siku ya Mama


MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake (UWT) Ilala, Nora Mzeru, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Mama iliyoandaliwa na Miss Earth, Bahati Chando, yatakayofanyika Mei 12, mwaka huu.

Siku hiyo itakuwa maalumu kwa mama na itawajumuisha wanawake wajasiriamali pamoja na wanawake wengine ambapo itafanyika katika Hoteli ya Lamada ya jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Bahati alisema wanawake wajasiriamali wataungana na wengine katika kufurahia siku hiyo, kubadilishana mawazo na kujengeneana uwezo katika masuala mengine ya ujasiriamali.

“Lengo la kufanya sherehe hizi ni kutaka wanawake kuungana kwa pamoja na wanawake wenzao duniani ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu katika kazi mbalimbali hasa zile za ujasiriamali kwa kuwa wanawake wanaweza,” alisema Bahati.

Aliongeza kuwa madhumuni ya maadhimisho hayo ni kutambua umuhimu wa mama, ambapo kaulimbiu ya mwaka huu ni: ‘Mara zote katika mioyo yetu inaonesha jinsi mama alivyo katika mioyo ya wote.’

No comments:

Post a Comment