Sunday 12 May 2013

Wanawake wajasiriamali wana nafasi ya kufanikisha biashara zao

Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania walioshiriki katika warsha ya wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, iliyoandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Dare to Dream na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania, Benki ya CRDB na kinywaji cha Malta. Warsha hiyo inayofanyika mara moja kwa mwaka ilifanyika jijini Dar es Salaam kwa kuwashirikisha wanawake zaidi ya 150.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakifuatilia moja ya mada zilizokuwa zikitolewa katika warsha ya wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, iliyoandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Dare to Dream na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania, Benki ya CRDB na kinywaji cha Malta. Warsha hiyo inayofanyika mara moja kwa mwaka ilifanyika jijini Dar es Salaam kwa kuwashirikisha wanawake zaidi ya 150.
Washiriki wa warsha ya wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, wakifungua warsha hiyo kwa kusali.
Washiriki wa warsha ya wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, wakifungua warsha hiyo kwa kusali.
Mkufunzi na mtaalamu wa maswala ya ujasiriamali, Bi. Rehmah Kasule, akitoa elimu kwa wanawake zaidi ya 150 juu ya kuwawezesha kujua mbinu za kujiendeleza katika kukuza biashara zao.
Msanii wa nyimbo za injili ambaye pia ni mjasiriamali, Bi. Elizabeth Benard, akiimba wimbo wa "anafanya jambo" katika warsha ya wanawake wajasiriamali zaidi ya 150.
Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Dare to Dream, Bi.Emelda Mwamanga, akifanyiwa mahojiano na waandishi wa habari juu ya warsha ya wanawake wajasiriamali iliyoandaliwa na taasisi yake na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania, Benki ya CRDB na kinywaji cha Malta.
Na Mwandishi wetu
WANAWAKE wajasiriamali wa Kitanzania wanayo nafasi nzuri ya kufanikiwa katika biashara zao ikiwa watajiamini na kuwa na uthubutu katika shughuli zao
Akizungumza wakati wa semina ya wanawake wajasiriamali iliyoambatana na maonyesho ya bidhaa mbalimbali jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Afisa mtendaji mkuu wa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Dare to Dream foundation iliyoandaa semina hiyo Emelda Mwamanga alisema kutojiamini ni moja kati ya sababu zinazowafanya wanawake wajasiriamali kushindwa kusonga mbele
Emelda alisema kuwa, duniani ya sasa ya kibiashara imejaa ushindani mkubwa na bila kujiamini itakuwa ni vigumu kwa wanawake wajasiriamali kuweza kufanikiwa.
"Semina hii imewaleta pamoja wanawake wa kada mbalimbali ili kuweza kubadilishana uzoefu pamoja na kutiana moyo. Wapo waliofanikiwa kibiashara ambao watawaeleza wale ambao bado hawajafanikia njia walizopitia mpaka kufika hapo walipo. Kupitia semina hii watajifunza na namna ya kutengeneza bidhaa zenye viwango pamoja na namna ya kujitanga," alisema
Kwa upande wake Afisa masoko wa benki ya CRDB Emmanuel Kiondo alisema kuwa benki yake inatambua umuhimu wa kumwezesha mwanamke na ndiyo maana ikaamua kujitokeza kudhamini shughuli hiyo iliyolenga kuwajengea uwezo wanawake
Tunaamini kuwa mwanamke akiwezeshwa familia nzima inakuwa imewezeshwa. Benki ya CRDB imekuwa ikimjali sana mwanamke na tumeweza kuanzisha akaunti ya Malkia maalumu kwa ajili ya wanawake wenye malengo mbalimbali ikiwemo ya kiujasiriamali," alieleza
Mwakilishi kutoka kampuni ya Vodacom ambao ndiyo wadhamini wakuu wa semina na maonyesho hayo Alice Lewis alisema Vodacom inatambua mchango wa wanawake katika maendeleo ya jamii na itaendelea kuwa mstari wa mbele kuwasaidia kusonga mbele.
Credit: Kapingaz

No comments:

Post a Comment