Tuesday 14 May 2013

Wanawake wahimizwa kutumia mitandao kutangaza biashara zao


Mkurugenzi wa kampuni Dare to Dream, Bi Emelda Mwamaga

WANAWAKE wajasiriamali wameshauriwa kutumia mitandao ya kijamii kutangaza biashara zao badala ya kuitumia kufanya mambo yasiyo na maana.

Ushauri huo ulitolewa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na Meneja wa Vodacom Foundation, Grace Lyon, katika mkutano wa tano wa uchumi wa wanawake wajasiriamali.

Akizungumza katika mkutano huo uliondaliwa na Kampuni ya Dare To Dream alisema: “Ni vizuri wafanyabiashara wakatumia mitandao ya kijamii ipasavyo katika kutangaza biashara zao sambamba na huduma ya M-pesa kwa ajili ya kuokoa muda wa kupanga foleni kwenye benki, mwanamke mjasiriamali akiwa mtumiaji wa huduma hii anakuwa katika hali ya usalama zaidi kwa fedha zake,” alisema Lyon.

Alisema huduma hiyo hivi sasa imepanuka kiasi cha kutoa huduma zaidi ya 200, hivyo alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wanawake wote nchini kujiunga.

Mkutano huo uliowakutanisha wanawake wajasiriamali uliambatana na mafunzo mbalimbali ya kukuza biashara pamoja na maonesho ya bidhaa mbalimbali.

No comments:

Post a Comment