Monday 13 May 2013

Tundu Lissu ahamasisha wanafunzi kupiga kura 2015


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgdf-fs9lRtAbwYc1sx08053pPBXaAQTnKlLQW1Bg_CEMPkk5OaZ8-CBtNfNJla1ddDXmvpfykg35TO_JPc9-dgmErBeIJ8iZJecUeXvkRxbOV7aa-U_xdYBH_kUykKiAv_79hbOxaTdAN7/s1600/tundu-lissu-2.jpg
Mhe. Tundu Lissu

MBUNGE machachari wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) amewataka wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mkwawa kutumia kura zao vizuri katika uchaguzi mkuu mwaka 2015 ili kuiondoa madarakani Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kutokana na kudidimiza uchumi na kutoleta maendeleo nchini.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara baada ya kualikwa na Jumuiya ya Wanafunzi wa CHADEMA walioko mkoani Iringa, Lissu alisema Serikali ya CCM imeshindwa kumkomboa mwananchi kutokana na wabunge na viongozi wake kutokuwa na uchungu na nchi.

Alisema ni kazi kubwa kwa sasa kwa mwananchi kupata maendeleo chini ya CCM, hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuitumia kura yake kuwachagua wabunge wengi wa upinzani na upande wa rais.

“Kila Mtanzania anajua kuwa utawala wa CCM ni giza tupu, angalieni maisha ya walimu, askari, wakulima na wafanyakazi, wako katika hali ngumu sana,” alisema.

Aidha, alitumia nafasi hiyo kumsifu Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa kwa kazi anayofanya katika kutetea maslahi ya taifa na Mkoa wa Iringa kwa ujumla kutokana na kusimama kidete bungeni.

No comments:

Post a Comment