Thursday 9 May 2013

Watanzania wahimizwa matumizi ya teknolojia

Mheshimiwa Raymond Mbilinyi


WATANZANIA wamehimizwa kujiwekea mikakati juu ya matumizi ya sayansi na teknolojia katika sekta mbalimbali za uzalishaji ili nchi ipige hatua za kiuchumi na kuboresha ustawi wa jamii.
Rai hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), Raymond Mbilinyi alipokuwa katika mkutano wa majadiliano ya ushirikiano wa manufaa ya wote (Smart Partinership Diologue) uliofanyika mjini Morogoro.
Mbilinyi Sayansi na Teknolojia ina nafasi kubwa ya kuleta maendeleo endelevu nchini hivyo watanzania waizingatie katika kuzitumia bila woga wala kusita.
Alisema hata Malaysia inayotamba kwa sasa kiuchumi imefika hapo ilipo kutokana na kuzingatia matumizi ya nyenzo hizo.
Mkutano huo ulifanyika kwa kushirikisha makundi ya wananchi kutoka mikoa ya Morogoro, Tanga na Pwani na ilihudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ambaye alishukuru serikali kupitia TNBC kwa kuleta fursa ya wananchi kuzungumzia na kujadili kwa uwazi masuala mbalimbali ya kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment